Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ubunge CUF hadharani Julai 17

28689 Cuf+pic Ubunge CUF hadharani Julai 17

Tue, 14 Jul 2020 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

CHAMA cha Wananchi (CUF), kimesema kinatarajia kuhitimisha kazi ya kura ya maoni kwa nafasi ya wagombea ubunge, Julai 17.

Akizungumza na Nipashe jana, Mkurugenzi wa Mipango na Uchaguzi wa CUF Taifa, Juma Kilaghai, alisema wameshaanza mchakato huo.

“Tumeshaanza mchakato wa kura ya maoni kwa wagombea wa nafasi za ubunge na kwa baadhi ya mikoa tumeshamaliza, ni maeneo machache tu ambayo yamebaki ambayo mpaka kufikia Julai 17 tutakuwa tumemaliza, ”alisema Kilaghai.

Pia, alisema kwa upande wa madiwani wameshamaliza kazi hiyo ya kura za maoni.

“Kwa madiwani tayari tumemaliza, tuna uhakika tutasimamisha madiwani zaidi ya asilimia 80 nchi nzima,” alisema Kilaghai.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live