Arusha. Shughuli ya kuandikishwa wapiga kura katika halmashauri ya wilaya ya Arusha mchini Tanzania inatarajiwa kuanza Julai 18 mwaka 2019, ambapo vituo 238 vimetengwa.
Akizungumza na Mwananchi leo Jumatatu Julai 15,2019 Mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Dk Wilson Mahela amesema taratibu zote muhimu za kuanza kwa shughuli hiyo zimekamika.
Mahela amesema ambao wanapaswa kujiandikisha ni vijana aliofikia umri wa miaka 18, wakazi ambao wamehamia jimbo la Arumeru Magharibi na wale watahitaji kurekebisha majina yao.
Ofisa uchaguzi jimbo la arumeru mashariki, Hadja Mkumbwa akizungumza katika semina ya waandikishaji katika daftari hilo, amewaka kufanyakazi kwa weledi na kuzingatia taratibu.
Amesema uandikishaji ni jambo la muhimu kwani wakikosea wao wameharibu juhudi zote za uandikishwaji na kupelekea kuharibu uchaguzi kwa ujumla.
"Hivyo tunawafundisha juu ya vitambulisho vilivyoharibika, fomu zitakazotumika pamoja na kutumia mashine za BVR," amesema
Pia Soma
- Mchungaji mbaroni kwa madai ya kumkashifu Museveni
- Bosi mpya TIB awatoa hofu wateja wa benki hiyo
- Bendi ya polisi yageuka kivutio, Kangi ajitosa kusakata muziki