Tue, 27 Jun 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, limelazimika kusimama ghafla baada ya Spika Tulia Ackson kuamuru wabunge watoke nje haraka.
Tukio hilo limetokea mapema leo Juni 27, 2023 wakati wa kipindi cha maswali na majibu ambapo ghafla zilisikika alam na ndipo Spika alipoamuru wabunge wote kutoka nje.
"Wabunge hali hiyo inaashiria tutoke bungeni haraka, hivyo nawaambia mtoke nje haraka na ninaahirisha shughuli za Bunge mpaka hali itakapokuwa sawa," alisema Spika Tulia.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live