Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Tanzania imesema Vyama vya TLP na UDP vilisitisha mpango wa kumuunga mkono Mgombea Urais wa CCM, Dkt. Magufuli kwasababu havikufuata Kanuni na Sheria za Uchaguzi.
Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa, Sisty Nyahoza amesema, waliwaambia TLP na UDP suala hilo lina utaratibu ambao walitakiwa kuufuata, na walipoona hawajafuata Vyama hivyo vimekaa kimya na havisikiki tena
Ameongeza, UDP wameendelea na kazi zao za kampeni, wakiwa na Mgombea wao na wanatangaza Sera za Chama chao. Aidha, TLP ambao waliweka mabango wameyatoa na wanaendelea na kampeni zao
Nyahoza amesema, “Kwa hiyo Vyama ni sikivu, vile ambavyo sio sikivu wawe wasikivu na kuzingatia Sheria na Kanuni maana kama Mgombea wa Chama chako asipokuwa msikivu, akishinda kwenye Uchaguzi itakuwaje?”