Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Sio mimi wala Lissu tuliozuia ndege, serikali ilikuwa inadaiwa sisi tulihoji – Zitto Kabwe

5793 Zitto TZW

Thu, 5 Apr 2018 Chanzo: bongo5.com

Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe amesema kuwa sio yeye wala Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu waliozuiwa ndege aina ya Bombardier Q400 iliyokuwa imezuiliwa nchini Canada isikamatwe.



Mh. Zitto amesema kuwa serikali ilikuwa inadaiwa hivyo wao walihoji tu na kuuliza maswali na hiyo ndiyo kazi yao kama upinzani kuendelea kuhoji.

Sio mimi wala ndugu Tundu Lissu tuliozuia ndege hii. Serikali ilikuwa inadaiwa na sisi tulihoji tu na kuuliza maswali. Ndio kazi yetu hiyo kama opposition na tutaendelea kuhoji. Mf. Nimeambiwa Serikali imelipa $63m kuokoa Hii ndege iliyokuja. Ndege mpya ni $31m. Tutahoji tu,” ameandika Zitto kupitia ukurasa wake wa Twitter.

Ndege iliyokuwa imezuiliwa nchini Canada ilikuja Tanzania Marchi 30 ikitokea Canada ilipokuwa imeshikiliwa.

Chanzo: bongo5.com