Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Sifa mgombea uchaguzi Serikali za mitaa kuwa kada wa CCM yasimamisha bunge dakika tatu

62607 Sifapic

Thu, 13 Jun 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dodoma.  Wabunge wa vyama vya upinzani leo Alhamisi Juni 13, 2019 bungeni jijini Dodoma wamesimama kwa takribani dakika tatu huku wakizomea na kupiga meza baada ya kuelezwa kuwa moja ya sifa ya wagombea katika uchaguzi wa Serikali za mitaa ni kuwa wanachama wa CCM.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango wakati akiwasilisha bajeti ya Serikali mwaka  2019/2020 ambayo ni Sh33.1 trilioni.

Wakati akihitimisha kuwasilisha kusoma bajeti hiyo, Dk Mpango aligusia uchaguzi huo utakaofanyika Oktoba 2019 kuwa ni kuchagua mtu anayetoka CCM.

"Sifa ya 10  awe anatoka ndani ya chama cha siasa kinachotetea maslahi na haki za wanyonge na chama hicho ni CCM, " amesema Dk Mpango.

Baada ya kauli hiyo ambayo Dk Mpango aliirudia mara tatu, wabunge wa upinzani walisimama huku wakipiga meza zao na kuimba "CCM, CCM, CCM. "

Wakati wapinzani wakiwa wamesimama,  wabunge wenzao wa CCM nao walisimama na kusababisha Dk Mpango kusimama kuwasilisha bajeti hiyo kwa dakika tatu.

Pia Soma

Spika Job Ndugai na kaimu mnadhimu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni,  Joseph Selasini walitumia nguvu ya ziada kuwatuliza wabunge wa pande zote mbili,  kumpa nafasi Dk Mpango kumalizia hotuba yake.

Dk Mpango alipopewa nafasi ya kuendelea kuwasilisha amesema alichokisema kina baraka ya Rais John Magufuli.

Chanzo: mwananchi.co.tz