Tue, 29 Jun 2021
Chanzo: ippmedia.com
Hata hivyo akiwa nje ya ukumbi wa Bunge, Bwege amepata nafasi ya kuzungumza na waandishi wa habari amesema, inawezekana akajiingiza tena katika kinyang'anyiro kwa kuwa siasa za Rais Samia ni tofauti na zilizopita.
“Kuna tofauti ya Bunge letu na hili, wingi wao naona hakuna uchangamfu wa bunge lakini wanajitahidi kwa sababu Mama Samia amewaambia waseme wanavyotaka kusema kwa hiyo wanajitahidi wanasema, kutokana na siasa ilivyobadilika inawezekana nikaingia tena kwenye kinyang’anyiro lakini ingekuwa siasa zile nisingeingia siasa za mama ni tofauti” - amesema Bwege.
Chanzo: ippmedia.com