Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Shaka amjibu Mbatia

Shakha Pic Data Shaka amjibu Mbatia

Mon, 3 Jan 2022 Chanzo: www.mwananchi.co.tz

Katie wa Itikadi na Uuenezi Shaka pia ametamka Mbatia kuelezea mikakati ya chama chake  ili kuwavutia wananchi  kujiunga na chama hicho kukubali na kusifu  kusifu hatua zinazochukuliwa na Serikali  ya awamu  sita .

Ameeleza hayo Januari 2, 2021 wakati akijibu madai mbalimbali ya Mbatia ambaye mapema jana alikutana na wanahabari na kuzungumza masuala mbalimbali ikiwemo kuwataka wananchi kutomshambulia Spika wa Bunge,  Job Ndugai kutokana na msimamo wake kuhusu Serikali kukopa.

SOMA: Mbatia ataka Ndugai asishambuliwe

Katika maelezo yake na wanahabari, Mbatia alisema kutofautiana kuhusu suala la kukopa kati ya Rais Samia Suluhu Hassan na Ndugai mjadala wao unaleta afya kwa sababu mihimili ya Bunge na Serikali inapokinzana ndio afya katika Taifa.

Mbatia alikwenda mbali zaidi na kutaka Ndugai asishambuliwe wala kutukanwa kutokana na msimamo wake kuhusu kukopa huku akiwataka watu kujadili hoja yake kwa mtazamo chanya na sio kumshambulia Ndugai binafsi.

Lakini Shaka amemtaka Mbatia kukinusuru chama chake ili kiwe chenye nguvu kitakachojadili nguvu ya hoja.

Amesema kupatia kutamka takwimu au kukosea  hakuwezi kumsaidia  mwananchi wa kawaida anayeishi vijijini.

Kuhusu suala la takwimu, Mbatia alisema itumike busara kwa Serikali kuomba radhi kuhusu takwimu zilizotangazwa na Rais Samia wakati akitoa salamu za kufunga na kuufungua mwaka mpya.

"Anapoonekana  kiongozi kama Mbatia aking'angania jambo  lisilo na msingi  wowote ni fedheha kwake na kwa chama chake.Wananchi  wasomi  na wenye maarifa wamekuwa wakiisifu utawala wa Rais Samia yakiwemo mataifa makubwa na taasisi za kimataifa.

Lakini Shaka amesema, "Kukosea kutaja takwimu au kupatia si hoja yenye maana na mashiko. Mbatia atazame kwanza utendaji wa Serikali jinsi unavyotekeleza majukumu ya kisera yanayoleta manufaa kwa jamii," amesema Shaka.

Shaka amesema kutamka takwimu kwa kupatia au kukosea haliwezi kugeuzwa ndio mjadala wenye  maana kwani kupatia au kukosea ni masuala ya kawaida na yasiyoweza kuzuilika kibinadamu

Chanzo: www.mwananchi.co.tz