Tue, 22 Aug 2023
Chanzo: mwanachidigital
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi (Bara), Joseph Selasini amesema sasa hivi lugha za hovyo zimekuwa nyingi na siyo demokrasia hivyo ameshauri kuwepo kwa tunu za Taifa za zitungiwe sheria.
Selasini ameyasema hayo leo Jumanne Agosti 22, 2023 katika mkutano wa kitaifa wa wadau kujadili hali ya demokrasia nchini kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwakani na Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025. ulioandaliwa na Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD).
Chanzo: mwanachidigital