Rais Samia amewaapisha viongozi Wateule aliowateua ambao ni Waziri Kinamba Waziri kuwa Mkuu wa Mkoa wa Njombe na Humphery Polepole kuwa Balozi wa Tanzania nchini Malawi.
Akiwaapisha viongozi hao leo Machi 15, 2022 Ikulu ya Chamwino Jijini Dodoma, Rais Samia amewataka wateule hao kuzingatia misingi ya uongozi na utumishi bora kwa manufaa ya taifa zima.
Akitoa maelekezo kwa Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Rais Samia amemtaka kusimamia ukusanyaji mapato ya mkoa, sambamba na taratibu za kupambana na janga la Corona ikiwa ni pamoja na kuhamasiha zoezi la uchomaji chanjo kwa wananchi.
Huku akiacha kiu kubwa kwa watu kuhusu maagizo yake kwa Balozi Polepole na kusema kuwa atazungumza nae pembeni mara baada ya kumaliza zoezi hilo la uapishaji.