Tue, 22 Jun 2021
Chanzo: ippmedia.com
Kikao hicho kimetanguliwa na kikao cha Secretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kilichofanywa na Katibu Mkuu wa CCM, Daniel Chongolo, katika ukumbi wa NEC Jijini Dodoma
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Juni 21, 2021 na Katibu wa Itikadi na Uenezi Shaka Hamdu Shaka, imesema kikao hicho kitaongozwa na Mwenyekiti wa CCM ambaye ni Rais Samia.
"Ni kweli Juni 22 2021 Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ataongoza kikao cha kawaida cha kamati Kuu, maandalizi yote yamekamilika, ni kikao cha kawaida cha Kikatiba," amesema Shaka.
Chanzo: ippmedia.com