Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rungwe aripoti Polisi Osterbay

61080 Pic+rungwe

Mon, 3 Jun 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Chama cha Umma (Chaumma) Hashim Rungwe ameripoti katika kituo cha polisi Osterbay kuitikia wito wa kamanda wa polisi Mkoa wa Kinondoni Mussa Taibu.

Rungwe amefika kituoni hapo saa 4.10 asubuhi ya leo Jumatatu Juni 3, 2019 akiwa amevalia kanzu nyeupe akiongozana na mtu mmoja ambao wote wameingia katika ofisi ya Kamanda Taibu.

Mwenyekiti huyo amefika kituoni hapo baada ya jana Jumapili Eugene Kabendera, kwa niaba ya Sekretarieti ya Ushirikiano wa Vyama nane vya Upinzani kutoa taarifa akisema polisi walifika katika ofisi za Chaumma jijini Dar es Salaam na kueleza Rungwe anatakiwa kuripoti leo Jumatatu Juni 3,2019 katika ofisi za Kamanda Taibu.

Katika mkutano huo, viongozi wa vyama hivyo walitoa tamko la kutoshiriki kwenye uchaguzi wa marudio kwenye kata 32 unaotarajiwa kufanyika  Juni 15, 2019 kwa sababu unasimamiwa na Wakurugenzi Halmashauri za wilaya na Manispaa kinyume na uamuzi wa Mahakama Kuu.

Wawakilishi wa vyama hivyo ni Wawakilishi wengine walikuwa wakitoka vyama vya Vyama vya ACT Wazalendo, CCK, Chadema, DP, NCCR Mageuzi, NLD na UPDP

Chanzo: mwananchi.co.tz