Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, leo Juni 7, 2022, amepokea hati za utambulisho kutoka kwa mabalozi wa nchi mbalimbali katika Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma. Rais Samia amepokea hati hizo na kufanya mazungumzo na Balozi Mteule wa Cuba hapa nchini Yordenis Despaigne Vera, Balozi wa Ethiopia Shibru Kedida, Balozi wa Shirikisho la Urusi Andrey Levonovish Avetsyan na Balozi Mteule wa Oman, Saud Hilal Al Shidhani.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, leo Juni 7, 2022, amepokea hati za utambulisho kutoka kwa mabalozi wa nchi mbalimbali katika Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma. Rais Samia amepokea hati hizo na kufanya mazungumzo na Balozi Mteule wa Cuba hapa nchini Yordenis Despaigne Vera, Balozi wa Ethiopia Shibru Kedida, Balozi wa Shirikisho la Urusi Andrey Levonovish Avetsyan na Balozi Mteule wa Oman, Saud Hilal Al Shidhani.