Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba amewataja viongozi na wanachama wengine waliofukuzwa uanachama katika mkutano mkuu uliofanyika kati ya Machi 13 hadi 15, 2019.
Licha ya jana Jumatatu Profesa Lipumba kulieleza Mwananchi kuwa Maalim Seif Sharif Hamad ni miongoni mwa waliofukuzwa kutokana na mwenendo wake wa kukidhoofisha chama hicho pia wamo wengine.
Soma zaidi: Huyu ndiye Profesa Lipumba wa CUF
Akizungumza na waandishi wa habari makao makuu ya CUF, Buguruni jijini Dar es Salaam leo Jumanne Machi 19, 2019, Profesa Lipumba amewataja wanachama wengine ni Ismail Jussa, Salim Biman, Issa Kheri, Mohammed Nur na Said Ali Mbarouk wote wa Zanzibar, Tanzania bara ni Mbarala Maharagande, Abdallah Katawi na Joran Bashange.
Hata hivyo, baadhi ya wanachama hao waliofukuzwa tayari leo Jumanne wamekabidhiwa kadi za chama cha ACT- Wazalendo akiwamo Maalim Seif.
Soma zaidi: Wabunge waliokuwa kwa Maalim Seif, waanza kurejea kwa Lipumba
Related Content
- Wabunge waliokuwa kwa Maalim Seif, waanza kurejea kwa Lipumba
- Zitto amkabidhi Maalim Seif kadi namba 1, Babu Duni namba 10
- CUF Pemba wataka bendera za ACT
- VIDEO: Wanaoshusha bendera za CUF, kupandisha za ACT waonywa
Profesa Lipumba ambaye ni mtaalamu wa uchumi, amewataka wanachama wa CUF hasa Zanzibar kuacha kufuata mkumbo kwenda chama kingine badala yake wabakie CUF ili kuijenga
"Msimfuate Maalim Seif bakini tuijenge CUF, tumetoka mbali hasa wanachama wa Pemba. Maalim Seif ni mharibifu na ameangukia ACT- Wazalendo ambayo ipo mahututi," amesema Profesa Lipumba.
Soma zaidi: Zitto amkabidhi Maalim Seif kadi namba 1, Babu Duni namba 10