Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Profesa Baregu afariki

DSC 1290 660x400.jpeg Profesa Baregu afariki

Mon, 14 Jun 2021 Chanzo: millardayo.com

Mwanachama wa CHADEMA na mwanazuoni, Prof. Mwesiga Baregu amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Jumapili Juni 13, 2021 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) alikokuwa akipatiwa matibabu.

Mkuu wa kitengo cha mawasiliano ya umma Muhimbili, Aminiel Aligaesha  amesema, “amefariki saa tano usiku wa kuamkia leo akiwa ICU (chumba cha uangalizi maalum)  na alikuwa hapo kwa takribani siku 15.”

Mkurugenzi wa Itikadi na Uhusiano wa kimataifa wa Chadema, John Mrema amesema chama kitatoa taarifa rasmi taarifa baada ya kikao na wanafamilia.

“Tunaelekea hospitali ya Muhimbili kukutana na wanafamilia halafu tutatoa taarifa rasmi,” Mrema.

BREAKING: MTANGAZAJI FREDWAA AFARIKI

Chanzo: millardayo.com