Aliyekuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Prof. Mussa Assad amesema Siasa inapelekea kutowekwa malengo yanayopimika katika Awamu za Utawala
Akizungumzia mwenendo wa siasa nchini, Prof. Assad amesema, "Kwa sababu ya Siasa hatujui malengo ni yapi, yanapimwa vipi na kwa wakati gani. Siasa kwa sehemu kubwa inatuharibia."
Aidha, akizungumzia sekta ya Kilimo akisema japokuwa Tanzania inatajwa kuwa Nchi ya Kilimo, mabwawa yapo katika Wilaya chache; "Ukitaka kuboresha kilimo, hakikisha una maji ya kutosha," amesema Prof. Assad.
Nini maoni yako kuhusu kauli ya mtaaluma huyu wa uchumi nchini?