Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Pinda amtaka Membe agombea urais kuleta ushindani

PINDA Pinda amtaka Membe agombea urais kuleta ushindani

Sun, 12 Jul 2020 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

WAZIRI Mkuu mastaafu Mizengo Pinda amemkaribisha aliyewahi kuwa kada wa Chama cha Mapinduzi, Bernard Membe kuwania nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwa ili kuleta ushindani wa kisiasa na kuwa ni haki yake ya kikatiba.

Akihojiwa na chombo kimojawapo cha habari nchini Pinda amesema kuwa ili mgombea ajisifie kushinda ni lazima awepo mtu wa kushindana naye.

"Unajua uzuri wa Chama cha Mapinduzi kina nguvu kubwa sana ,kwa hiyo kama kuna mtu anataka kugombea kwanza anakaribishwa kwa kuwa ni haki yake ,Membe mimi ni rafiki yangu sana" amesema Pinda.

Uchaguzi Mkuu wa Urais wabunge na madiwani unatarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu na tayari vyama mbalimbali vipo katika michakato ya ndani ya kuandaa wagombea wao kwa nafasi mbalimbali.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live