Dodoma. Waziri Mkuu mstaafu wa Tanzania, Mizengo Pinda amewaasa wajumbe wa mkutano mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dodoma kuchagua kiongozi asiye na makundi kwani yamekuwa yakikimaliza chama hicho.
Pinda ambaye ni mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM ametoa kauli hiyo leo Jumamosi Machi 7, 2020 wakati akizungumza kwenye mkutano wa uchaguzi wa Mwenyekiti wa chama hicho wilaya ya Dodoma Mjini.
Amesema makundi siku zote yanakimaliza CCM na kuwagawa wanachama jambo alilosema linawagharimu kwa kiasi kikubwa wanachama.
CCM Dodoma kinafanya uchaguzi huo ikiwa imepita miezi miwili tangu alipotimukiwa madarakani mwenyekiti wake Robert Muwinje katika sababu ambazo zinatajwa ni kukiuka kanuni.
"Tunapozungumzia suala la usafi ni vigumu sana kumpata mtu wa aina hiyo, lakini msichague mtoa rushwa na kikubwa zaidi msilete mtu mwenye kugawa makundi maana hiyo ndiyo mbaya zaidi," amesema Pinda.
Mjumbe huyo amewataka wana CCM kumchagua mtu ambaye yuko tayari kwa ajili ya kukifia chama na mwenye kujitoa zaidi kwa ajili ya chama chake kwa wakati huu.
Pia Soma
- Asasi 23 Tanzania zalilia usawa wa kijinsia kwenye uchaguzi mkuu
- Wenye watoto Albino wapewa somo kuelekea uchaguzi mkuu Tanzania
- CRDB yahamashisha usawa wa kijinsia katika
- Tatizo la ajira Tanzania latawala mdahalo wa Vijana ACT- Wazalendo