Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ninakwenda bungeni kulia – Mgombea ubunge kupitia CHADEMA

1845 Picsalummwalimu TZW

Thu, 25 Jan 2018 Chanzo: bongo5.com

Mgombea ubunge katika Jimbo la Kinondoni kupitia tiketi ya CHADEMA, Salum Mwalimu amesema kuwa akifanikiwa kuchukua jimbo hilo basi atakuwa mwendawazimu bungeni katika kutetea maslahi ya wananchi wake.

Salum Mwalimu 

Mwalimu ambaye ni Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA Zanzibar amedai kuwa jimbo hilo limekuwa nyuma kimaendeleo kitu ambacho kimeondoa hadhi yake pamoja na watu wake na kuahidi kuwa atapigania kwa hali na mali kuweza kurudisha heshima ya jimbo hilo kwa kulilia vitu muhimu serikalini ili kurudisha hadhi ya Kinondoni.

Ninakwenda bungeni kulia, ninakwenda bungeni kuwa mwendawazimu kwa ajili ya mahitaji ya watu wa Kinondoni,“amesema Salum Mwalimu jana kwenye mkutano wake na Waandishi wa Habari.

Hata hivyo, Mwalimu amesema kuwa jimbo hilo linachangamoto nyingi ikiwemo ubovu wa miundo mbinu, Changamoto za huduma ya Afya na kuahidi kuwa kero hizo zitakwisha kwani yupo tayari kupigania maslahi ya watu wa Kinondoni.

Chanzo: bongo5.com