Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ndugai bega kwa bega na wabunge ACT Wazalendo

Bbc8c33fb00e5270e4a8fae961526331 Ndugai bega kwa bega na wabunge ACT Wazalendo

Wed, 16 Dec 2020 Chanzo: habarileo.co.tz

Baada ya leo kuwaapisha wabunge wateule wa chama cha ACT Wazalendo, Spika wa Bunge, Job Ndugai amewahakikishia kuwa atawahapa ushirikiano na kusikiliza maoni na ushauri wao.

Akizungumza katika viwanja vya bunge jijini Dodoma, Spika Ndugai amesema atahakikisha analinda haki za wabunge hao ikiwemo kuwasikiliza, kupokea maoni na ushauri wao.

“Ni wajibu wa Spika kuhakikisha walio wachache wanapata haki ya kusikilizwa na kama hoja itakuwa nzito basi walio wengi wataamua lakini haki ya kusikilizwa itakuwepo,” amesema Ndugai.

Aidha, amesema Kwa kutambua kuwa watanzania wanapenda kusikia bajeti zikipangwa kwa kutoa, basi watafanya hivyo kwa weledi na kufanya maamuzi bora kwa maslahi ya taifa.

“Uchaguzi umeisha, uchaguzi ule wa Oktoba 28 umekwisha, sasa tusonge mbele, tufanye kazi tukimsaidia Rais kwa maslahi ya taifa hili”ameongeza Ndugai

Amesema hadi sasa kuna idadi ya wabunge 383 ambao wameampishwa, bado wabunge 10 ili kolamu ya bunge itimie na kufanya maamuzi.

Wabunge hao 10 ni wale watano ambao ni wa kuteuliwa na Rais, na watano ni wale wanaotoka Baraza la Wawakilishi Zanzibar.

Chanzo: habarileo.co.tz