Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ndugai asalimu amri, asema.....

Video Archive
Mon, 3 Jan 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai amesema katika hotuba yake aliyoitoa hivi karibuni hakukuwa na hapakuwa na jambo la kukashifu wala kudharau juhudi za Serikali bali alikuwa anasisitiza ulipaji wa kodi na tozo mbalimbali.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatatu Januari 3, 2022 jijini Dodoma, Ndugai amesema “Katika mazungumzo yale baadaye ikatengenezwa clip na baadhi ya watu wakakatakata mambo, wakawasilisha ujumbe nusu, ujumbe nusu ule umesababisha mjadala mkubwa katika nchi yetu, ambao mjadala umesababisha usumbufu wa hapa na pale” amesema Ndugai nakuongeza

“Kwa hiyo niliona tukutane pamoja na mambo mengine niweke sawa jambo hilo lilivyokuwa, hapakuwa na lolote la kukashifu wala kudharau juhudi zozote za Serikali, tunahitaji Serikali na tunaiunga mkono”

“Katika mazungumzo yetu niliwataka wenzetu pamoja na mabo mengine tulipe kodi, ushuru na tozo mbalimbali huo ndio ulikuwa msisitizo wa hotuba yangu” amesema

Chanzo: www.tanzaniaweb.live