Mon, 13 Jun 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Naibu Spika, Mussa Azan Zungu amewaonya wabunge kuzingatia nidhamu pamoja na kuacha kuwakatisha wachangiaji kwa kutoa taarifa ambazo nyingi hazina msingi bali zinamtoa mbunge kwenye mtiririko wake.
“Kuanzia mjadala wa bajeti kuu hapatakuwa tena na taarifa za mchezo humu ndani. Hivi karibuni wabunge wamekuwa wakilalamika mnawaingilia flow [Mtiririko] zao za kuchangia, taarifa zimekuwa nyingi si taarifa za maana, bali taarifa za kupotezeana muda,” amesema.
Hata June 14 Bunge litajadili Bajeti Kuu ambayo itakuwa ikiwasilishwa na Waziri wa Fedha, Dk. Mwigulu Nchemba.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live