Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC imewataka wasimamizi wa uchaguzi kuhakikisha wanasimamia taratibu za uchaguzi ili haki itawale.
Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Huduma za Kisheria wa NEC, Emmanuel Kavishe wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa wasimamizi wa uchaguzi kutoka katika majimbo ya Bumbuli, Same na Monduli yanayofanyika mkoani Tanga.
Alisema kuwa wanajukumu la kuhakikisha wanafanikisha chaguzi ndogo zinatarajiwa kufanyika katika maeneo mbalimbali ya nchi mnamo Mwezi Mei.
"Niwaase acheni kufanya kazi kwa mazoea au kufanya upendeleo kwa watu fulani au chama fulani, mkahakikishe mnakwenda kusimamia chaguzi zinafanyika katika misingi ya uhuru na haki," alisema Kavishe.
Hata hivyo Kaimu Katibu Tawala wa mkoa wa Tanga, Sebastiani Masanja aliwataka kuzingatia maelekezo watakayopewa katika mafunzo hayo kwani watakwenda kuyafanyia kazi kipindi cha uchaguzi utakapofika.