Dar es Salaam. Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza uchaguzi mdogo wa udiwani katika kata 13 za Tanzania Bara utakaofanyika Agosti 17, 2019.
Taarifa ya tume hiyo iliyotolewa jana Ijumaa Agosti 2, 2019 inaeleza kuwa utoaji wa fomu za wagombea ulipangwa kuanza Julai 29 hadi leo Jumamosi Agosti 3, 2019 ambapo pia utafanyika uteuzi wa wagombea.
Inaeleza kuwa hadi jana saa 10 jioni wagombea 58 wa vyama vya siasa 18 walichukua fomu za uteuzi.
Vyama ambavyo wagombea wake wamchukua fomuĀ na idadi yao katika mabano ni Demokrasia Makini (5), AAFP (5), CCK (3), DP (4), SAU (4), UDP (4), ACT-Wazalendo (2), UPDP (5), ADC (2), TLP (1), CCM (12), Ada Tadea (4), Chadema (2), Chaumma (1), NRA (1), NLD (1), CUF (2) na UMD mmoja.