Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

NEC yaanza maandalizi uchaguzi 2025

Kuraaa.png NEC yaanza maandalizi uchaguzi 2025

Wed, 3 May 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Serikali imesema Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ipo katika maandalizi ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 na hivyo itagawa majimbo ya uchaguzi kwa kuzingatia taratibu na vigezo vilivyoainishwa katika sheria wakati wa kugawa majimbo utakapofika.

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge Ummy Nderiyananga ameliambia Bunge jijini Dodoma kuwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi itatoa tangazo rasmi kwa wadau wote wa uchaguzi juu ya kuanza kwa machakato wa ugawaji wa majimbo ili wadau wawasilishe maoni na maombi yao ambayo yatashughulikiwa kwa mujibu wa vigezo vilivyowekwa kikatiba.

Naibu Waziri Ummy alikua akijibu maswali ya Mbunge wa Kilindi Omar Kigua aliyetaka kujua ni lini Serikali italigawa jimbo la Kilindi lililopo wilyani Kilindi mkoani Tanga.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live