Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mwenisongole awekwa mtu kati na Wabunge wanawake

Bungeni 660x400 Wabunge wanawake mshukia Mwenisongole

Thu, 2 Jun 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mbunge wa Mbozi, George Mwenisongole ameingia katika mgogoro na wabunge wanawake kutokana na lugha aliyoitumia kutafsiriwa kuwa ilikuwa ya kuudhi.

Mbunge huyo amelazimika kufuta kauli yake aliyosema kuwa baadhi ya mawaziri waliopeleka wake zao siku za kusoma hotuba kwamba walikwenda kuuza sura bungeni.

Akichangia hotuba ya makadilio ya mapato na matumizi kwa Wizara ya Nishati leo Alhamisi Juni 2, 2022, mbunge huyo alimpongeza Waziri January Makamba kwamba kitendo cha kutompeleka mke wake wakati wa kusoma hotuba yake kilionyesha umakini mkubwa katika kazi yake.

Mwenisongole amesema baadhi ya watu walikuwa wakipeleka wake zao siku walizokuwa wanasoma hotuba za bajeti zao na akasema kwamba wanawake hao walikuwa wanakwenda kuuza sura bungeni.

Kauli ya mbunge huyo iliwaamsha wabunge, Ruth Mayenga na Ester Matiko ambao kwa nyakati tofauti waliamua kutoa taarifa kwa mujibu wa Kanuni za bunge wakimtaka mbunge huyo kufuta kauli yake kwani inawadhalilisha wanawake.

“Mheshimiwa Mwenyekiti, hii siyo lugha nzuri, ni lugha ya maudhi humu ndani, hakuna mwanamke ambaye anakuja huku kwa ajili ya kuuza sura, wale wanakuja kwa mwaliko maalumu ya wenza wao ambao wanawapenda,” amesema Matiko.

Advertisement Ombi la wabunge hao lilikubaliwa na Mwenyekiti wa bunge ndipo akamtaka mchangiaji huyo kufuta kauli yake ndipo aendelee na mchango wake jambo lililokubaliwa na Mwenisongole.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live