Thu, 16 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Mwanza, akiwemo mwandishi wa habari, Gerald Robert wamechukua fomu ya uenyekiti wa CCM wa mkoa huo.
Uchaguzi huo utafanyika kuziba nafasi ya Sixbert Jichabu aliyeteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Masasi mkoani Mtwara.
Ukiacha mwanahabari huyo, wengine waliochukua fomu ni Hamidu Said ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Mirongo, ambapo pia yupo Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Sengerema, Mark Augustino.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live