Akikabidhi nyumba hiyo amesema kuwa nyumba hiyo, ikishafanyiwa maboresho, itakuwa Ofisi ya Mkoa wa Kichama wa Selou, wenye majimbo ya Namtumbo, Tunduru Kaskazini na Tunduru Kusini.
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Ado Shaibu amempongeza Mtutura kwa moyo wa kujitolea uliouonyesha
Mtutura aliyewahi kuwa Mbunge wa Tunduru Kusini kupitia CCM, kabla ya kuhamia ACT Wazalendo mwaka jana.
Ado amesema tokea Mtutura ajiunge na chama hicho akitokea CCM, amekuwa akichukua hatua mbali mbali za kukiimarisha chama katika mkoa wa Kichama Selous.
Mbali na Katibu Mkuu na Katibu wa Mkoa wa Selou, wengine walioshiriki katika mapokezi hayo ya nyumba itakayotumika kama moja ya ofisi za chama mkoani humo ni Katibu wa jimbo la Tunduru kaskazini Mchungaji Francis Kavele na Katibu wa Ngome ya Wanawake Gania Shamte.