Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Msajili ailima barua nyingine Chadema

83188 Pic+msajili

Fri, 8 Nov 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Msajili wa vyama vya siasa nchini Tanzania amekiandikia barua Chadema kukitaka kuwasilisha ratiba ya mkutano mkuu wa kuchagua viongozi wa kitaifa wa chama hicho kabla ya Novemba 11, 2019.

Barua hiyo imetolewa leo Jumatano Novemba 6, 2019 na naibu msajili wa vyama vya siasa, Sisty Nyahoza kwa niaba ya msajili wa vyama vya siasa, Jaji Francis Mutungi.

Oktoba Mosi, 2019 chama hicho kikuu cha upinzani  nchini Tanzania kiliandikiwa barua na ofisi hiyo wajieleze kwanini wasichukuliwe hatua kwa madai ya kukiuka Sheria ya Vyama vya Siasa kwa kuchelewa kufanya uchaguzi mkuu wa chama hicho.

Chama hicho kilijibu barua hiyo ya msajili kwa hoja sita.

Katika barua hiyo msajili amesema lengo la kutaka maelezo hayo ni kurahisisha ofisi ya msajili kutekeleza majukumu yake.

“Pamoja na mambo mengine, ratiba hiyo ionyeshe tarehe ya kutoa fomu za kugombea kwa wanachama wenye nia ya kugombea, tarehe ya uteuzi wa wagombea na uchaguzi.”

Pia Soma

Advertisement
“Taarifa hiyo iwasilishwe ofisi ya msajili siyo zaidi ya Novemba 11 2019 saa 9:30 alasiri,” inaeleza sehemu ya barua hiyo.

Nyahoza alipoulizwa kuhusu barua hiyo amesema imetolewa na ofisi ya msajili, kwamba ni mwendelezo wa barua ya Oktoba Mosi, 2019.

Katibu mkuu wa Chadema, Dk Vicent Mashinji amelieleza Mwananchi kuwa hajapata barua hiyo, “nipo katika kikao sijaiona barua yenye maudhui hayo.”

Kifungu cha 4 (5) (b) cha Sheria ya Vyama vya Siasa sura ya 258 (RE.2019) kinaipa ofisi hiyo mamlaka ya kufatilia uchaguzi na uteuzi wa viongozi wa vyama vya siasa ili kuhakikisha unafanyika kwa mujibu wa sheria hiyo, katiba na kanuni za chama husika.

Chanzo: mwananchi.co.tz