Sun, 7 Jan 2018
Chanzo: bongo5.com
Mbunge wa Kibamba, John Mnyika na Naibu Katibu Mkuu Bara baada ya kwenda kumtembelea Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu amesema hakika Mungu ni mkubwa.
Mnyika amesema kuwa tabasamu la Mbunge huyo ni maumivu kwa waliopanga mauaji.
“Hakika Mwenyezi Mungu ni mkubwa. Tabasamu kama hili ni maumivu kwa waliopanga mauaji. Rais @MagufuliJP aruhusu wachunguzi wa kimataifa waje wafichue ukweli,” aliandika Nyika kupitia mtandao wake wa Twitter.
Mnyika aliongozana na wanachama na viongozi mbali mbali wa Chama cha Demokrasia (Chadema)alifika jana Nairobi hospital kumjulia hali Mbunge huyo.
Chanzo: bongo5.com