Thu, 31 May 2018
Chanzo: bongo5.com
Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amempongeza aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana huku akimkaribisha na kumpa hongera aliyechukua nafasi yake, Dkt. Bashiru Ally.
Dkt. Kikwete pia amempongeza Mwenyekiti wa Chama hicho, Dkt.John Pombe Magufuli.
“Kwa heri Kinana. Hongera kwa kazi nzuri. Daima tutakukumbuka. Hongera Bashiru. Nakutakia kila la heri. Hongera @ccm_tanzania , hongera Mwenyekiti @MagufuliJP Umoja ni Ushindi, Kidumu Chama Cha Mapinduzi !,” ameandika Kikwete kupitia ukurasa wake wa Twitter.
Loading...
Chanzo: bongo5.com