Sun, 23 Sep 2018
Chanzo: mwananchi.co.tz
Bukoba. Mgombea udiwani wa CCM Kata ya Kagondo Dk Anatory Amani amepita bila kupingwa baada ya vyama vya upinzani kutokuweka mgombea udiwani kwenye kata hiyo.
Msimamizi wa uchaguzi wa kata hiyo, Veda Kyaishozi amemtangaza leo Septemba 22, 2018 na kumkabidhi barua kama diwani mteule wa kata hiyo.
Baada ya kukabidhiwa barua hiyo Dk Amani amesema
wanachama wa CCM walijiandaa kupambana kwa ajili yake ili kupata ushindi na kubainisha kuwa yupo tayari kuwatumikia.
Chanzo: mwananchi.co.tz