Mgombea Ubunge jimbo la Ngorongoro kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Emmanuel Shangai ameibuka kidedea katika uchaguzi mdogo uliofanyika kufuatia kifo cha aliyekuwa Mbunge na Naibu Waziri wa Uwekezaji, William Ole Nasha.
Mgombea Ubunge jimbo la Ngorongoro kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Emmanuel Shangai ameibuka kidedea katika uchaguzi mdogo uliofanyika kufuatia kifo cha aliyekuwa Mbunge na Naibu Waziri wa Uwekezaji, William Ole Nasha. Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Ngorongoro Dk. Jumaa Mhina amemtangaza Shangai kuwa Mbunge Mteule wa Jimbo hilo baada ya kupata kura 62,017 dhidi ya wagombea wenzake wa ACT Wazalendo aliyepata kura 170 na Saimon Ngilisho wa Demokrasia Makini aliyepata kura 105.