Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mfanyabiashara abambwa na doti 600 za CCM

KANGA CC.png Mfanyabiashara abambwa na doti 600 za CCM

Sun, 5 Jul 2020 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Mkoa wa Shinyanga, imemkamata mfanyabiashara wa magari ya teksi, Joseph Tasia, akiwa na doti 600 za vitenge vyenye nembo ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) nyumbani kwake na kushindwa kutoa maelezo yanayojitosheleza.

Mkuu wa Takukuru mkoani humo, Hussein Mussa, katika taarifa yake jana alisema mtuhumiwa huyo alikamatwa Juni 29, saa 3:00 usiku mtaa wa Mwasele B.

Mussa alisema walimkamata Tasia akiwa na doti hizo zikiwa zimehifadhiwa nyumbani kwake jambo ambalo linaashiria kuwa zilikuwa zinaandaliwa kutumika katika kufanya ushawishi kwa wapigakura.

"Uchunguzi wa Takukuru mkoani Shinyanga umebaini Tasia mfanyabiashara wa magari madogo ya teksi hana duka wala hafanyi biashara ya kuuza vitenge," alisema.

Aidha, alisema katika mahojiano alishindwa kutoa maelezo yanayotosheleza kuhusiana na mzigo huo aliokutwa nao na hata nyaraka za ununuzi alizowasilisha hazijitoshelezi, hivyo kuonyesha shaka juu ya uhalali wake.

"Uchunguzi wa kina wa tukio hili unaendelea ili kubaini iwapo vilikuwa kwa ajili ya kuhusiana na vitendo vya rushwa katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba, mwaka huu au ni kwa ajili ya kufanya biashara katika msimu huu," alisema.

Mussa alisema ofisi hiyo inawaonya watu wote wenye nia ya kutumia taarifa zozote za uchunguzi zinazofanywa nao kwa nia ya kujinufaisha kisiasa kwani kitendo hicho ni kuingilia uchunguzi na ni kosa la jinai na atakayebainika atachukuliwa hatua," alisisitiza.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live