Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mdee, Bulaya na Matiko watoka jela

98755 PIC+MDEE Mdee, Bulaya na Matiko watoka jela

Fri, 13 Mar 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es salaam. Wabunge watatu wa Chadema  wametoka gereza la Segerea leo Jumatano Machi 12, 2020 baada ya jana kushindikana kutokana na sababu mbalimbali.

Wabunge hao ni Esther Matiko (Tarime Mjini), Ester Bulaya (Bunda) na Halima Mdee (Kawe).

Viongozi wanane wa Chadema pamoja na aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Vicent Mashinji Jumanne Machi 10, 2020 walihukumiwa kulipa faini ya Sh350 milioni au kwenda jela miezi mitano baada ya kutiwa hatiani kwa makosa 12 kati ya 13 yaliyokuwa yanawakabili.

Washtakiwa hao wakiongozwa na mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe walilazimika kwenda jela baada ya kushindwa kukamilisha taratibu za kulipa faini hiyo waliyohukumiwa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Baada ya hukumu hiyo iliyosomwa  na Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, Chadema walianza kuchangishana fedha kwa ajili ya kuwalipia faini viongozi wake hao.

Hadi jana mchana Chadema walikuwa wamechangisha Sh234 milioni na kutumia Sh110 milioni kuwalipia wabunge hao watatu ambao jana ilishindikana kutoka, sasa wametoka leo. CCM walimlipia Dk Mashinji Sh30 milioni na alitoka jana.

Habari zinazohusiana na hii

Advertisement
Waandishi wa Mwananchi walioweka kambi katika gereza la Segerea kuanzia saa 1 asubuhi walishuhudia wabunge hao wakitoka katika mazingira ambayo yalikuwa vigumu kuwapata na kuzungumza nao kutokana na wingi wa askari wa  Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU).

 

Chanzo: mwananchi.co.tz