Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mdee Acharuka: Serikali Ilipe Deni

Mdee?fit=851%2C476&ssl=1 Mdee Acharuka: Serikali Ilipe Deni

Sat, 17 Apr 2021 Chanzo: globalpublishers.co.tz

Mbunge wa Viti Maalum, Halima Mdee, ameitaka Serikali kulipa deni inalodaiwa katika Mifuko ya Hifadhi za Jamii ili Wastaafu walipwe kwa wakati.

Akiwa Bungeni leo, Mdee amesema Duniani kote Mifuko ya Jamii huisaidia Serikali kufanya shughuli za maendeleo kwa kukopa kwa riba na kulipa, lakini kwa Tanzania Serikali na Taasisi zake zinakopa kwa riba lakini hazilipi.

Amebainisha kuwa, Hotuba ya Waziri Mkuu inaonesha kuunganishwa kwa Mifuko mwaka 2018 kumeongeza ufanisi, ubora na kupunguza gharama za uendeshaji.

Ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Serikali (CAG) inaonesha Deni la Serikali ni Tsh. Trilioni 2.7 lakini haijajumuisha Tsh. Trilioni 1.7 za PSSF.

Chanzo: globalpublishers.co.tz