Thu, 20 Apr 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mbunge wa Jimbo la Nkasi, Aida Kenan amedai kubaguliwa kwenye utendaji wa kazi jimboni kwake ambapo wakuu wa idara na watumishi wote wa Nkasi wamepigwa marufuku na mkuu wa mkoa kumpa ushirikiano wowote.
Kenan ameyasema hayo April 20, 2023 bungeni jijini Dodoma na kueleza kwamba ameandika barua kwa mawaziri husika mara kadhaa kuhusu jambo hilo lakini halijafanyiwa kazi.
Amedai kuwa hali hiyo inafanya wananchi wa Nkasi kukosa haki zao za msingi na yeye kukosa haki zake za kufanya kazi kwa ufanisi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live