Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mbunge Katani asema hafikirii kuondoka leo wala kesho

27327 KATANI+PIC TanzaniaWeb

Sat, 17 Nov 2018 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dodoma. Mbunge wa Tandahimba (CUF), Katani Ahmed Katani (CUF) amekanusha madai ya kujiuzulu ubunge na ameomba vyombo vilivyomnukuu kumuomba radhi haraka.

"Sifikirii kujiuzulu leo, wala kesho na hata siku yoyote labda wanaotumika waje wanifukuze wenyewe," amesema Katani

Katani ametoa kauli hiyo bungeni leo jioni Alhamisi Novemba 15, 2018 baada ya taarifa kusambaa kwamba amejizulu.

Amesema haijui hiyo barua inayotajwa kuandikwa na yeye na akasema kitendo hicho kimemdhalilisha.

Hotuba yake imekatizwa na Spika Job Ndugai baada ya kelele nyingi za kumshangilia kutoka kwa wabunge wa upinzani ndipo Spika akaomba makatibu wake wamsaidie kubaini sauti ya mbunge mwanamke aliyekuwa akipiga kelele zaidi.

Katani ataendelea kuchangia baadaye baada Spika Ndugai kumpata aliyepiga kelele na kutoa uamuzi.

Endelea kufuatilia Mwananchi



Chanzo: mwananchi.co.tz