Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mbunge Chadema ataka mkataba Star Media na TBC kuvunjwa, Waziri Mwakyembe amjibu

Mbunge Chadema ataka mkataba Star Media na TBC kuvunjwa, Waziri Mwakyembe amjibu

Fri, 31 Jan 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dodoma. Mbunge wa Tarime Mjini (Chadema) nchini Tanzania, Esther Matiko ametaka mkataba wa kampuni ya Star Media na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kuvunjwa kwa sababu umekuwa ukijiendesha kwa hasara tangu ulipoingiwa mwaka 2009.

Esther aliyasema hayo jana Alhamisi Januari 30, 2020 bungeni jijini Dodoma wakati akichangia taarifa za kamati ya Bajeti na ile ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma (PIC).

Esther alisema kampuni hiyo ilianza na mtaji wa Sh547 bilioni walisema ikifika 2014 wangeweza kutoa gawio lakini kinyume chake inajiendesha kwa hasara.

Alisema mwaka wa fedha 2014/15 walipata hasara ya Sh6.8 bilioni na kwamba cha kushangaza mtaji mwaka 2018 ni hasi ya Sh119 bilioni.

Hata hivyo, alisema Serikali ya Tanzania bado inaendelea kulikumbatia shirika hilo kama mbia na kwamba cha kushangaza hata ukitaka kuunda kamati teule kufuatilia unazuiliwa.

“Tunataka kujua kuna nini nyuma ya Star Media. Fedha za Watanzania asilimia 35 zimewekezwa pale kama wabia, tunataka kujua ni kwa nini mkataba huu usisitishwe, naomba muuvunje huu mkataba,” alisema.

Pia Soma

Advertisement
Akijibu hoja hiyo, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo wa Tanzania, Dk Harrison Mwakyembe alisema taarifa mbili za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na kamati maalum iliyoundwa naye kuchunguza mkataba huo imeibua madudu mengi sana.

“Madudu ya jinai tumewakilisha kwa vyombo husika vya Serikali, ya kiutendaji tumeyafanyia marekebisho, kwa mara ya kwanza Star Media imeweza kuchangia Sh500 milioni mfuko mkuu Hazina,” alisema Dk Mwakyembe.

Alisema pia Star Media imekubali upungufu uliosababishwa na baadhi ya watendaji wake watailipa TBC Sh3 bilioni kuanzia Machi 2020.

Alisema mambo yanaenda vizuri na kwamba maelezo zaidi atayatoa katika siku za usoni.

Chanzo: mwananchi.co.tz