Dodoma. Mbunge wa Ulanga (CCM) nchini Tanzania, Goodluck Mlinga amesema kutokana na ukosefu wa usafiri katika Gereza la Ulanga mkoani Morogoro, askari wamekuwa wakitumia bodaboda kuwasafirisha mahabusu kwenda mahakamani.
“Nilini Serikali itapeleka gari katika gereza la Ulanga,” amehoji Mlinga.
Kabla ya kumruhusu Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni kujibu, Spika wa Bunge, Job Ndugai akasema, “hii ni mpya kama mambo haya yapo.”
Akijibu, Masauni amesema watatatua changamoto ya ukosefu wa magari kadri yatakapopatika na kwamba yakipatikana watapeleka katika gereza la Ulanga.
Naye Mbunge wa Tarime Mjini (Chadema) Esther Matiko amehoji ni lini Serikali itapeleka nguo kwa ajili ya wafungwa.
Amesema katika gereza la Segerea jijini Dar es Salaam kutokana na kukosekana kwa nguo, jambo ambalo limesababisha askari wa magereza kuwapa nguo zao wanapotoka nje.
Pia Soma
- Rais Magufuli apokea hati za utambulisho mabalozi tisa
- Virusi vya Corona vyaanza kusambaa duniani, 106 wafariki China
- Mbunge CCM asema barabara ya Mvumi Dodoma imeoza, Serikali yamjibu