Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mbunge CCM adai shambulio la Lissu ni mpango wa Chadema

40881 MORELIPIC Mbunge CCM adai shambulio la Lissu ni mpango wa Chadema

Mon, 11 Feb 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dodoma. Mbunge wa Siha (CCM), Dk Godwin Mollel amesema tukio la Tundu Lissu kushambuliwa kwa risasi zaidi ya 30 jijini Dodoma ni mpango uliosukwa na Chadema na kutoa sharti kwa chama hicho kikuu cha upinzani nchini Tanzania kuwa wakilitimiza atakuwa tayari kuthibitisha.

Dk Mollel, mbunge wa zamani wa Siha kwa tiketi ya Chadema aliyejiunga CCM mwaka 2018 na kupitishwa kuwania ubunge na kuibuka na ushindi, ametoa kauli hiyo leo Ijumaa Februari 8, 2019 bungeni jijini Dodoma.

Amesema hata siku ya kufanya uchunguzi baada ya Lissu kupigwa risasi, kuna baadhi ya sampuli aliziiba lakini uongozi wa Chadema ulikataa pendekezo lake la kupeleka sampuli hiyo Afrika Kusini kufanya uchunguzi kwani walikuwa na hofu ya kuumbuliwa.

“Mimi nilikuwa huko lakini nilikimbia kwa mipango yao,  hata katika tukio la kushambuliwa Lissu mimi niliingia ndani kwenye uchunguzi na niliiba baadhi ya vitu lakini wakakataa mapendekezo yangu," amesema Mollel.

Hata hivyo, mbunge wa Tunduma (Chadema), Frank Mwakajoka aliomba taarifa akimtaka Dk Mollel kueleza ni kwa nini alikuwa anakiuka kiapo cha udaktari, na mbunge huyo wa Siha kujibu kuwa alifanya hivyo kwa sababu alikuwa kada mwaminifu wa Chadema.

Wakati Mwakajoka akieleza hayo, mbunge wa Rombo (Chadema), Joseph Selasini alimtaka Dk Mollel kuthibitisha madai yake kuhusu Lissu.

Katika majibu yake Dk Mollel amesema hawezi kuthibitisha hadi Chadema watakapomueleza fedha za ruzuku zinakwenda wapi na mpango waliotaka kuufanya kwa Zitto Kabwe (mbunge wa Kigoma Mjini) na marehemu Chacha Wangwe, walipotaka kugombea uenyekiti wa Chadema.

Soma Zaidi: Alichokisema dereva wa Lissu katika mahojiano Ujerumani



Chanzo: mwananchi.co.tz