Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mbowe mgeni rasmi Siku ya vijana duniani

NTOBI 1 Mbowe mgeni rasmi Siku ya vijana duniani

Sun, 24 Jul 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) taifa, Mhe. Freeman Mbowe anatarajiwa kuwa Mgeni rasmi katika Maadhimisho ya Siku ya Vijana Duniani yatakayofanyika Mjini Shinyanga Agosti 12,2022.

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari leo Jumapili Julai 24,2022 Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi CHADEMA mkoa wa Shinyanga, Mhe. Emmanuel Ntobi amesema maandalizi ya Maadhimisho ya Siku Vijana duniani ambayo kitaifa mwaka huu yanafanyika mkoani Shinyanga yanaendelea vizuri.

Ntobi ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Maadhimisho ya Siku ya Vijana Duniani mkoani Shinyanga amesema mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA taifa, Freeman Mbowe akiambatana na Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika.

“Tunapenda kuujulisha umma wa watanzania kuwa maadhimisho ya siku ya vijana duniani iliyoanzishwa na Umoja wa Mataifa mwaka 2020 kwa mara ya kwanza nchini Tanzania inafanyika mkoani Shinyanga katika ukumbi wa Lyakare Hotel ambapo tunaratajia kupokea wageni zaidi ya 4000 kutoka ndani na nje ya nchi”,amesema Ntobi.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live