Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe amewavua uongozi Mwenyekiti wa Chama hicho na kamati yake ya utendaji Wilaya ya Tanga kwa kile kilichodaiwa kuwa wanawajibishwa ili kutoa nafasi ya kupata viongozi watakaokwenda na kasi ya chama hicho.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe amewavua uongozi Mwenyekiti wa Chama hicho na kamati yake ya utendaji Wilaya ya Tanga kwa kile kilichodaiwa kuwa wanawajibishwa ili kutoa nafasi ya kupata viongozi watakaokwenda na kasi ya chama hicho. Waliovuliwa uongozi ni Nuru Athumani aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Tanga, Grace Mtote aliyekuwa Katibu wa chama hicho Wilaya ya Tanga pamoja na wajumbe wote wa kamati ya utendaji ya Wilaya ya Tanga.