Hai. Mbunge wa Hai (Chadema), Freeman Mbowe amewasili katika viwanja vya Nkoromu kata ya Masama Kati kwenye mkutano wa hadhara na kupokelewa na mamia ya wananchi.
Leo Ijumaa Februari 28, 2020 Mbowe ameanza ziara ya ya siku tano katika jimbo hilo kuzungumza na kusikiliza kero za wananchi.
Katibu wa Chadema Wilaya ya Hai, John Munis amesema polisi wamewapa kibali cha kufanya mikutano hiyo.
“Mbowe atazungumza na wananchi wake pamoja na kusikiliza kero mbalimbali zinazowakabili. Mikutano hiyo itafanya kwa siku tano mfululizo, kuanzia leo Ijumaa hadi Jumanne ijayo katika sehemu mbalimbali za Wilaya ya Hai,” amesema Munis.
Kamanda wa polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Salum Hamduni amesema polisi wana taarifa ya mkutano huo.
'”Kiutaratibu mbunge anapokuwa na mikutano yake anapaswa kutoa taarifa kituo cha polisi wilaya na taarifa za mkutano wa Mbowe tunazo,” amesema Kamanda Hamduni.
Pia Soma
- Mbowe akamatwa na polisi, asema anapitia kipindi kigumu
- VIDEO: Uteuzi wa wagombea ACT- Wazalendo watangazwa
- Mwanyika wa Acacia na wenzake watimiza siku 498, gerezani bila upelelezi kukamilika