Mmwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freemon Mbowe amesema jamii imekuwa haifuati uzazi wa mpango unaotakiwa, ili kwenda na kasi ya ukuaji kiuchumi.
Amesema kwa mujibu wa tafiti, zimeeleza kuwa vijana millioni 1.4 kila mwaka wanatakiwa kuingia kwenye soko la ajira, akisema kuwa pia vijana asilimia 50 ni chini ya umri wa miaka 18, hivyo wanatakiwa wapewe elimu itakayoendana na soko la ushindani wa ajira.
Mbowe aliyasema hayo kwenye kongamano la maadhimisho ya Siku ya Vijana Duniani lililofanyika Kanda ya Serengeti kitaifa kwenye makao yake makuu mkoani Shinyanga, iliyojumisha pia mikoa ya Simiyu na Mara.