Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mbowe: Hatutasusa uchaguzi, hatutokubali kuchakachuliwa matokeo

80146 Chadema+pic

Tue, 15 Oct 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Chama Kikuu cha Upinzani nchini Tanzania cha Chadema kimesema hakitasusia uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika Novemba 24, 20919 na hakitaruhusu kuchakachuliwa kwa matokeo.

Kauli hiyo imetolewa leo Jumanne Oktoba 15, 2019 na Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari makao makuu ya Chadema, Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Mbowe aamesema hawatoruhusu matokeo ya uchaguzi huo kuvurugwa na vyombo vya dola wala watumishi wa serikali.

Amesema japokuwa wamefungwa mikono kwa miaka minne kwa kutokufanya siasa watashiriki uchaguzi huo na wana uhakika watashinda.

“Wakijaribu kuvuruga au kuchakachua uchaguzi huu tutawatuma wananchi, serikali itambue kuwa wananchi wana ghadhabu,” amesema Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni

“Watanzania waache uoga, hatuwezi kuingiza uoga, tukategemea tutabadilisha nchi haya ni mapambano ya kisiasa wacha watumie mbinu zao zote, sisi tutatumia nguvu ya umma kuhakikisha kuwa tunashinda,” amesema

Habari zinazohusiana na hii

Advertisement

Chanzo: mwananchi.co.tz