Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mbowe: Chadema ikishika usukani Lugha itakuwa Kingereza

Mbowepic Siasa Leo Mbowe Chadema

Thu, 7 Apr 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mjadala wa lugha gani itumike kufundishia katika mfumo wa elimu, mara nyingi umekuwa ukiibua hisia mbalimbali miongoni mwa wadau wa elimu nchini.

Aghalabu mitazamo huwa ni miwili, ama Kiingereza kiendelee kutumika kama ilivyo sasa katika ngazi za sekondari na vyuo vya elimu ya juu, au tugeukie Kiswahili ambacho kwa sasa kinatumika katika ngazi ya elimu ya msingi pekee.

Mitazamo hiyo imezaa kambi mbili kuu kubwa ambazo mara zote zimekuwa zikiparurana kwa hoja.

Hivi karibuni, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alitoa msimamo wa chama chake, akisema kikifanikiwa kushika dola, lugha itakayotumika ni Kiingereza ili kuondoa alichokiita ubaguzi wa kiajira unaotokana na vijana wengi wa Kitanzania kutoijua lugha hiyo.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live