Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Maneno ya Mzee Makamba kwa Rais Magufuli ‘2020 mshindi ni CCM, wewe lala’

351 Hqdefault 1 TZW

Tue, 19 Dec 2017 Chanzo: bongo5.com

Katibu Mkuu wa zamani wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Yusuph Makamba amemuambia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli kuwa mwaka 2020 mshindi wa CCM hivyo amemuasa alale.

Akiongea leo katika Mkutano Mkuu wa 9 wa CCM alipopewa nafasi ya kuzungumza amesema kuwa Rais Magufuli ahitaji kwenda kwa Prof. Maji Marefu kupiga ramli kujua mshindi nani.

“Nyumba inajengwa na msingi na msingi wa CCM na nchi hii umejengwa na wazee wetu Nyerere na Karume hivyo walichokifanya wazee Mwinyi, Mkapa na wengineo ni kujenga matofali kama ambavyo amefanya Jakaya Kikwete na unavyofanya Rais Magufuli,” amesema Yusuph Makamba.

“Kwa ubatizo huu wa moto, 2020 mshindi ni CCM, wewe lala, hauhitaji kwenda kwa prof. Maji Marefu kupiga ramli kujua mshindi nani.Kuna mtu alikufananisha na nabii Nehemia lakini mimi nakufananisha na Yohana mbatizaji.”

Chanzo: bongo5.com