Katibu wa NEC -Itikadi na Uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa Ndugu Paul Christian Makonda ameanza rasmi ziara ya Kichama yenye Lengo la kukagua na Kusikiliza kero mbalimbali na kuzitafutia Ufumbuzi.
Ndugu Makonda leo Januari 19 amepokelewa kwa kishindo katika ofisi za chama Kinondoni tayari kwa ziara hiyo ya kuzunguka mikoa 20 back to back kabla ya kuelekea Bagamoyo mkoa wa Pwani.
Makonda ameanza Awamu ya pili katika Mkoa wa Pwani Wilaya ya Bagamoyo kusikiliza kero na kuzitafutia Ufumbuzi kama ambavyo amefanya Awamu ya kwanza kuizunguka Kanda ya Ziwa iliyoleta Mafanikio makubwa ndani ya Chama kwani alipokea na kutatua kero mbalimbali za Wananchi.