Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Makonda: Lissu mjanja kawakimbia Chadema

Makonda: Lissu Mjanja Makonda: Lissu mjanja kawakimbia Chadema

Fri, 19 Jan 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo Ndg. Paul Makonda amebainisha kuwa Tundu Lissu ni mjanja ndio maana ameamua kuwakimbia CHADEMA baada ya kuona hakuna haja ya kufanya maandamano yasiyo na tija wala maana yoyote na kuamua kwenda zake Nchini Ivorycoast kuangalia mpira katika mashindano ya AFCON.

Mwenezi Makonda ameyasema hayo leo tarehe 19 Januari, 2024 kwenye Mkutano wa hadhara akizungumza na Wananchi wa Jimbo la Kawe Jijini Dar es salaam.

Akizungumza na Wananchi hao, Mwenezi Makonda amewataka Watanzania kuwauliza CHADEMA kwanini wanamkimbia kwenye kuitisha mdahalo na badala yake wanaleta masharti na sababu ambazo haziingiliani kwenye mdahalo juu ya kile wanachotaka kukifanya cha kuandamana.

Makonda amesema kuwa CHADEMA wamekuwa wakifanya vikao ambavyo hawatoi mrejesho kwa wanachama wao wala wananchi na tafsiri yake hata maoni yao wanayosema wametoa kwa wananchi si ya wananchi bali ni yao wenyewe Mbowe, Lissu na Mnyika.

Pia, Mwenezi Makonda amewataka tena Mbowe, Lissu na Mnyika kufanya mdahalo wa kuzungumza ilikusudi wananchi kuelewa na kuchagua upande wao kuandaman au kutoandama na kukemea tabia ya Chadema kuwabuluza Wananchi kwa ajenda zao

Chanzo: www.tanzaniaweb.live